LIVE STREAM ADS

Header Ads

NSSF YAWAPA NAFUU WAAJIRI, YAWATAKA KUCHANGAMKIA MSAMAHA WA TOZO

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Alisema ukuaji huo umechangiwa na ongezeko la wanachama na michango, uwekezaji wenye tija, mazingira mazuri ya uwekezaji pamoja na matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma.

Alieleza kuwa kupitia mifumo ya TEHAMA, waajiri na wanachama sasa wanaweza kufuatilia na kuwasilisha michango, kufuatilia madai ya mafao na kupata huduma mbalimbali bila kulazimika kufika katika ofisi za NSSF.

Kuhusu ulipaji wa mafao, Bw. Mshomba alisema Mfuko umeendelea kuboresha mifumo yake ambapo kwa sasa mafao mengi hulipwa ndani ya siku 20, tofauti na siku 60 zinazotakiwa kisheria.

“Lengo letu ni kuhakikisha mwanachama anapata stahiki zake kwa wakati. Endapo kuna ucheleweshaji mara nyingi chanzo huwa ni mwajiri kutowasilisha michango kwa wakati,” alisema.

UWEKEZAJI WENYE TIJA, SKIMU YA HIFADHI KUONGEZA WANUFAIKA

Akizungumzia uwekezaji, alisema NSSF inaendelea kutekeleza miradi ya kimkakati inayochangia ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira, akitolea mfano Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi ambacho kimeendelea kuongeza uzalishaji, kutoa ajira na kuwawezesha wakulima wanaokizunguka.

Kuhusu Skimu ya Hifadhi, Bw. Mshomba alisema mpango huo umewezesha wananchi waliojiajiri kujiunga na mfumo wa hifadhi ya jamii na kunufaika na mafao mbalimbali ikiwemo pensheni ya uzee, pensheni ya ulemavu, pensheni ya urithi, mafao ya uzazi, msaada wa mazishi pamoja na huduma za matibabu.

“Tunawahimiza waliojiajiri kujiunga kupitia Skimu ya Hifadhi kwa sababu mpango huu unabadilisha maisha yao na kuwapa uhakika wa kunufaika na mafao mbalimbali. Lengo letu ni kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa Staa wa Mchezo katika kujilinda dhidi ya changamoto za maisha,” alisema Bw. Mshomba.

Alisema NSSF itaendelea kushirikiana na waajiri, wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kuimarisha mfumo wa hifadhi ya jamii nchini na kuhakikisha unaleta manufaa kwa Watanzania wengi zaidi.

No comments:

Powered by Blogger.