LIVE STREAM ADS

Header Ads

TANZANIA NA RWANDA KUSHIRIKIANA KATIKA SEKTA YA SHERIA

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa BMG Media. Mawasiliano +255 757 432 694 ama ripotabmg@gmail.com
Tanzania na Rwanda zimekubaliana kushirikiana katika sekta ya sheria, ikihusisha utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala, uthibiti wa uhalifu unaovuka mipaka pamoja kuimarisha huduma za msaada wa kisheria kwa wananchi.

Makubaliano hayo yamefikiwa katika mazungumzo kati ya Waziri wa Katiba na Sheria wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, na Waziri wa Masuala ya Sheria na Mwanasheria Mkuu wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Dkt. Emmanuel Ugirashebuja.

Nchi hizo zimekubaliana kubadilishana uzoefu na maarifa katika utatuzi wa migogoro, kukabiliana na uhalifu unaovuka mipaka na kuimarisha upatikanaji wa huduma za kisheria kwa wananchi, hususan wenye uhitaji.

Ushirikiano huu unaonesha dhamira ya Tanzania na Rwanda katika kuimarisha utawala wa sheria, mifumo ya haki na upatikanaji wa haki kwa wananchi wa nchi hizo mbili.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi za Wizara ya Sheria ya Rwanda jijini Kigali, yakihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Dkt. Seif Shekalaghe, pamoja na Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria kwa Umma, Ndg. Obadia Kameya.

No comments:

Powered by Blogger.